Sinopsis
Makala ya kila siku yanayompa fursa msikilizaji kutoa maoni yake juu ya habari zilizopewa uzito wa juu kwa siku husika. Msikilizaji hushiriki kwa kutuma ujumbe mfupi pamoja na kupiga simu.
Episodios
-
Watu karibu 500 wakamatwa nchini Kenya kufuatia maandamano ya Juni 25 2025
02/07/2025 Duración: 10minWanatuhumiwa kwa mauaji, ugaidi, ubakaji na makosa mengine. Wanaharakati wa haki za binadamu, wanasema, wanawake 14 walibakwa wakati wa maandamano hayo.
-
-
Mkataba kati ya DRC na Rwanda ya kuleta amani yakudumu mashariki mwa DRC
30/06/2025 Duración: 09minUmoja wa Afrika umekaribisha makubaliano yaliyotiwa saini mwishoni mwa juma lililopita kati ya Rwanda na DRC, hatua ambayo itashuhudia unyang'anyaji wa silaha na kuondolewa kwa mamluki wa kigeni mashariki mwa Congo.
-
-
Hatua ya bunge la Uingereza kuruhusu huduma ya kusaidiwa kufa
26/06/2025 Duración: 09minBunge la Uingereza hivi majuzi liliidhinisha mswada wa huduma ya kusaidiwa kufa
-
Maandamano ya kumbikizi ya kuwauwa kwa vijana zaidi ya 60 mwaka jana
25/06/2025 Duración: 10minWaandamanaji wakabiliana na polisi siku nzima wakati ya maandamano ya kuwakumbuka watu waliopoteza maisha wakati wa maandamano ya mwaka jana ya Gen Z
-
Zambia :Rais Hakainde Hichilema asisitiza serikali kufanya mazizi ya Edgar Lungu
24/06/2025 Duración: 10minRais wa Zambia Hakainde Hichilema ameendelea kusisitiza kufanya mazishi ya kitaifa kwa mtagulizi wake Edgar Lungu Licha ya mzozo uliopo baina yake na familia juu ya utekelezwaji ya matakwa ya marehemu ya kukataa kufanyiwa mazishi ya kitaifa.Tunakuuliza maoni yako kuhusu mzozo huo.
-
MAONI: DRC na Rwanda zitie saini makubaliano kumaliza mauaji ya raia
20/06/2025 Duración: 10minKila siku ya Ijumaa, hapa RFI Kiswahili, tunampa mskilizaji wetu nafasi kuzungumzia habari kuu ambazo tumekuwa nazo wiki hii au kutueleza jambo lolote ambalo limetokea nchini mwake. Wiki hii maoni mseto yameangazia, miongoni mwa taarifa zingine, tangazo kwamba Rwanda itatia saini makubaliano na DRC tarehe 27 Juni, kumaliza mapigano mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, lakini pia mashambulio baina ya Israeli na Iran.
-
Burundi : Rais Ndayishimiye ataka mazungumzo na upinzani
16/06/2025 Duración: 10minRais wa Burundi Evariste #Ndayishimiye ametoa wito kwa upinzani kushiriki katika mazungumzo na chama chake CNDD-FDD baada ya uchaguzi wa wiki iliyopita ambao ulikumbwa na upinzani mkubwa kwa ukosefu wa uwazi. Hata hivyo upinzani haujaonyesha nia ya kushiriki mazungumzo hayo. Tunakuuliza, ni sahihi upinzani kujiunga na serikali ? skiza makala haya kuskia maoni ya mskilizaji.
-
Utumwa wa watoto waendelea kuripotiwa licha ya juhudi mbalimbali zinazowekwa
13/06/2025 Duración: 09minJuni 12, ni Siku ya Kimataifa ya Kupinga Ajira kwa Watoto. Inakadriwa, takriban watoto milioni 200 kote duniani wanatumikishwa badala ya kuwa shuleni. Tunakuuliza, serikali yako inafanya vya kutosha kukomesha utumwa wa watoto? Unamfahamu mtoto anayefanyishwa kazi?
-
Kwa nini wanaume wanashindwa kutafuta ushauri wa afya ya akili
13/06/2025 Duración: 10minMakala haya yanaangazia afya ya akili, ikizingatiwa kuwa Juni ni Mwezi wa Uhamasishaji wa Afya ya Akili ya Wanaume. Unafikiri ni kwanini wanaume wanashindwa kutafuta ushauri wa afya ya akili? Unadhani afya ya akili ya mwanaume inasahaulika? Skiliza makala ya leo usikie maoni kutoka kwa waskilizaji wetu.
-
Rwanda yajiondoa ndani ya muungano wa mataifa ya Africa ya Kati
09/06/2025 Duración: 09minLeo shaba yetu inalenga nchi ya Rwanda ambapo nchi hiyo imetangaza kujiondoa kwenye Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika ya Kati, na kuituhumu jirani wake DRC, kwa kutumia baadhi ya wanachama kuendeleza ajenda zake zinazokandamiza Rwanda. Skiza makala hay kuskia maoni ya mskilizaji wetu.
-
Maoni ya waskilizaji wetu Juma hili
31/05/2025 Duración: 09minKila Ijumaa rfi Kiswahili inakupa nafasi ya kuchangia mada yoyote iwe kila uliskia kwenye habari zetu au kile kinachoendelea hapo ulipo. Skiza maoni ya mskilizaji.
-
Uganda : Ombi la Msamaha wa rais Museveni ni la kweli
29/05/2025 Duración: 09minLeo shaba yetu inalenga taifa la Uganda ambapo rais Yoweri #Museveni pamoja na mkewe wameomba raia wa nchi hiyo msamaha kwa mabaya yote ambayo serikali yao imetekeleza kwa miaka 39. Je, unafikiri kauli ya Rais Museveni na Mama Janet kuomba msamaha ni ya kweli au ni ya kisiasa?Skiza maoni ya mskilizaji wetu.
-
EAC : Je wanachama wana cha kujivunia
28/05/2025 Duración: 09minKatika makala haya shaba yetu inalenga jumuia ya Africa mashariki, tumekuuliza mskilizaji je unahisi una chochote cha kujivunia kuwa mwanachama wa jumuiya ya Africa Mashariki. Skiza maoni ya mskilizaji wetu.
-
Africa: Ina lolote cha kujivunia
27/05/2025 Duración: 09minUmoja wa Afrika imesherekea siku ya kiafrika, kuadimisha kuundwa kwa Umoja wa Afrika, kipindi hiki nchi ya Uganda nayo ikisitisha ushirikiano wake wa kijeshi na taifa la Ujerumani. Kuna chochote bara la Afrika linaweza kujivunia?Ndilo swali tumekuuliza, skiza makala haya kuskia maoni ya waskilizaji.
-
DRC: Kabila kuondolewa kinga je ni sahihi
26/05/2025 Duración: 09minKwenye makala haya tunajadili kilichotokea nchini DRC ambapo bunge la seneti lilimuondolea kinga ya kutoshtakiwa rais wa zamani, Joseph Kabila, hatua ambayo sasa inatoa nafasi kwa mahakama ya kijeshi kumshtaki kiongozi huyo kwa tuhuma za uhaini. Unazungumziaje hatua hii ya seneti, unadhani ilikuwa sahihi?Ndio swali tumekuuliza?skiza maoni ya baadhi ya waskilizaji.
-
Maoni ya waskilizaji kuhusu habari zetu juma hili
23/05/2025 Duración: 09minIlivyo ada kila siku ya ijumaa rfi Kiswahili hukiupa nafasi kuchangia chochote kile, maana yake nini? unachangia chochote kile, ulichoskia kwenye habari zetu au kile kinachoendelea hapo ulipo. Skiza makala haya kuelewa zaidi.
-
Mazungumzo ya Kigali na Washington kuhusu Rwanda kuwapokea wahamiaji kutoka Marekani
22/05/2025 Duración: 10minLeo hii tunaangazia Mazungumzo kati ya nchi ya Rwanda na Marekani kuhusu Kigali kuwapokea wahamiaji haramu watakaofukuzwa kutoka Washington. Unazungumziaje mazungumzo haya sawia na kauli ya mashirika ya Kimataifa ya kutetea haki za binadamu yakiongozwa na Amnesty International, yanayosema mpango huo utakiuka haki za wakimbizi?Skiliza kauli mbalimbali katika makala ya leo.
-
Uganda yapitisha mswada kuruhusu raia kushtakiwa kwenye mahakama ya kijeshi
21/05/2025 Duración: 09minWabunge wa upinzani hata hivyo walisusia kikao kilichopitisha mswada huo kwa haraka. Wanasiasa wa upinzani wanadai mswada huo unawalenga wakosoaji wa rais Yoweri Museveni