Sinopsis
Makala ya Wimbi la Siasa inakupa fursa ya kufahamu masuala ya kisiasa yanayoendelea ndani na nje ya Bara la Afrika. Kwenye Makala haya utapata habari ambazo zinakugusa moja kwa moja wewe msikilizaji. Kila wakati usikose kusikiliza Makala ya Wimbi la Siasa
Episodios
-
Je, maazimio ya jumuiya za EAC na SADC kuhusu DRC yatatekelezwa ?
12/02/2025 Duración: 10minMakala ya Wimbi la Siasa wiki hii tunaangazia maazimio ya wakuu wa serikali na nchi kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki na SADC waliokutana Februari jijini Dar es Salaam, kuthathmini hali ya usalama Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.Miongoni mwa maazimio hayo ni usitishwaji wa vita bila masharti kati ya waasi wa M23 na wanajeshi wa DRC na kutoa wito wa mazungumzo.Wachambuzi wetu ni Chube Ngorombi akiwa Goma, na Francois Alwende akiwa jijini Nairobi.
-
Nini hatima ya Afrika baada ya Trump kusitisha misaada ?
05/02/2025 Duración: 10minRais wa Marekani Donald Trump, baada ya kurejea madarakani Januari 20, ametangaza hatua ya serikali yake, kusitisha misaada hasa ya kifedha kwa nchi za kigeni, kupitia Shirika la Misaada ya Kimataifa (USAID).Hatua hii inamaanisha nini hasa kwa mataifa ya Afrika ? Tunajadili hili kwa akina na Suba Churchil, rais wa kituo cha taifa cha mashirika ya kiraia akiwa jijini Arusha Tanzania.
-
Nini suluhu ya mzozo wa Mashariki mwa DRC ?
29/01/2025 Duración: 10minWiki hii mapigano makali yameshuhudiwa jijini Goma, kati ya wanajeshi wa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na waasi wa M 23 wanaoripotiwa kuungwa mkono na nchi ya Rwanda. Nini suluhu ya mzozo wa Mashariki mwa DRC ?
-
Rais Samia ateuliwa na cham chake kuwania urais mwaka 2025
22/01/2025 Duración: 10minRais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ameteuliwa kwa kauli moja na wajumbe wa chama cha mapinduzi CCM kupeperusha bendera ya chama hicho wakati wa uchaguzi mkuu mwezi Oktoba. Tunachambua hatua hii.