Sinopsis
Makala ya Wimbi la Siasa inakupa fursa ya kufahamu masuala ya kisiasa yanayoendelea ndani na nje ya Bara la Afrika. Kwenye Makala haya utapata habari ambazo zinakugusa moja kwa moja wewe msikilizaji. Kila wakati usikose kusikiliza Makala ya Wimbi la Siasa
Episodios
-
Mgogoro kati ya rais na naibu wake nchini Kenya ambao ni mzozo wa kihistoria
23/10/2024 Duración: 10minHatma ya aliyekuwa naibu rais wa Kenya Rigathi Gachagua sasa utaamuliwa na mahakama baada ya mabunge yote mawili kumwondoa madarakani kwa njia ya hoja maalum Hatua ya kuondolewa Gachagua ni dhihirisho ya kuvunjika kwa uhusiano kati ya rais William Ruto na naibu wake Gachagua ,matukio ambayo si mageni nchini Kenya.
-
Maadhimisho ya mwaka mmoja wa shambulio la Hamas huko Gaza Oktoba 7 2024
09/10/2024 Duración: 10minMakala wimbi la siasa inaangazia maadhimisho ya kumbukumbu ya mwaka mmoja tangu kundi la Hamas, litekeleze shambulio baya zaidi kuwahi kutekelezwa huko Israeli, tukio ambalo lilianzisha vita ambayo imesababisha vifo kwa maelfu ya raia wa Kipalestina na maandamano duniani kote kupinga vita hiyo, wakati huu mzozo huo ukihofiwa kuenea katika mashariki ya kati. Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka na waalikwa wake
-
Visa vya utekaji na mauaji ya wanasiasa wa upinzani Afrika Mashariki
11/09/2024 Duración: 10minMakala ya Wimbi la siasa inaangazia tukio la kutekwa na kuuawa, kwa wanasiasa wa upinzani kwenye nchi za Afrika mashariki,tukio la hivi punde likiwa ni kutekwa kwa mwanasiasa mwandamizi wa chama cha upinzani nchini Tanzania cha Chadema Ali Kibao, na baadaye alikutwa ameuawa, na matukio haya yanaripotiwa pia nchini Uganda na DRC. Ungana na Ruben Lukumbuka pamoja na waalikwa wake Jawadu Mohamed ni mchambuzi na mtaalamu wa siasa za Tanzania akiwa Daresalaam Tanzania, pia Frankline M wa CMD nchini Kenya.
-
Mzozo wa Ethiopia na Somalia na mchango wa jumuiay aza kikanda kutuliza hali
06/09/2024 Duración: 09min