Habari Za Un

17 FEBRUARI 2025

Informações:

Sinopsis

Hii leo jaridani tunaangazia hali ya kibinadamu kwa wakimbizi na raia wa Sudan, na maradi wa lishe bora kwa watotot nchini Kenya. Makala inatupeleka nchini Tanzania na mashinani nchini Zambia, kulikoni?Kutokana na hali tete ya kibinadamu nchini Sudan, Umoja wa Mataifa na wadau wake leo Februari 17 jijini Genea, Uswisi, wamezindua mipango ya misaada ya kibinadamu na wakimbizi kwa mwaka huu 2025 kwa Sudan, wakihitaji jumla ya dola bilioni 6 kusaidia karibu watu milioni 26 ndani ya Sudan na kanda nzima.Mradi unaoendeshwa na serikali ya kenya  na kupigwa jeki na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF ambao ni wa kuboresha lishe kwa watoto kwa kugawa fedha taslim na elimu ya afya au NICHE (NISHI) umeleta nuru kwa wakazi wa Lokichar katika kaunti ya Turkana Kaskazini Mashariki mwa Kenya na miongoni mwa wanufaika ni Leah Akiru.Katika makala Assumpta Massoi kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO nchini Tanzania anakuletea mnufaika wa mafunzo ya ufugaji bora wa mbuz